• KIBAYACLASSIC

    The voice of Africa

    Thursday, May 4, 2017

    OBAMACARE KUFUTILIWA MBALI NA BUNGE

    Image result for USA PARLIAMENT
    Bunge la wawakilishi Marekani limepanga kura leo kufutilia mbali sheria ya huduma ya afya ya nafuu unaojulikana kama Obamacare.
    Wanachama wa Republican wana imani kwamba sasa wana kura za kutosha.
    Kevin McCarthy, kiongozi wa wengi bungeni amesema kwamba hatua muhimu imepigwa kuelekea kuidhinishwa mojawapo ya ahadi alizotoa rais Donald Trump wakati wa kampeni.
    Kipengee kilichokarabatiwa kinachoahidi dola bilioni 8 kusaidia watu walio na magonjwa ya kitambo, kinaonekana kuwaridhisha waliokuwa na shaka.
    Jitihada ya awali kufutilia mbali sheria hiyo mnamo Machi haikufaulu na ilikuwa mojawapo ya wakati mgumu wa siku mia moja za kwanza za rais Trump katika utawala.

    No comments:

    Post a Comment