• KIBAYACLASSIC

    The voice of Africa

    Friday, May 5, 2017

    KENYA IMEZINDUA KIFAA CHA KUJIPIMA VVU.


    Image result for AIDS
       Kenya imezindua kifaa cha bei nafuu cha kujipimia virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, ambacho raia wataweza kukitumia bila usaidizi wa daktari.
    Kifaa hicho kitaanza kutolewa kwa umma mwezi Julai mwaka huu.
    Kifaa hicho kinalenga watu 400,000 ambao hawajafahamu iwapo wana Virusi Vinavyosababisha Ukimwi au la.
    Wataalamu wanasema kwamba, kifaa hicho kinafanikiwa asilimia 80, na kitagharimu kama dola 7 hivi na kitapatikana katika maduka ya kuuzia madawa.
    Ili kujipima, mtu anatoa mate, damu au majimaji kutoka mwilini na kisha anajipima binafsi bila ya kusaidiwa na mtu.
    Martin Sirengo, kiongozi mkuu wa shirika la kukabiliana na Ukimwi Kenya, Nascop, anasema kuwa bado watu watahitajika kwenda hadi katika vituo vya matibabu ili kuthibitisha matokeo.


    No comments:

    Post a Comment