• KIBAYACLASSIC

    The voice of Africa

    Monday, February 12, 2018

    HUYU NDIYE MSHINDI WA TUZO YA UTAWALA BORA AFRIKA.

    Image result for Ellen Johnson Sirleaf

    Rais wa zamani wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ameshinda tuzo ya mwaka ya Mo Ibrahim kwa Uongozi wa Afrika - ambayo hupewa viongozi wa Afrika ambao wameonekana kuwa na utawala mzuri.
    Ellen Johnson Sirleaf amekuwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kushika nafasi ya Urais mwaka 2006 na kumaliza muda wake mwezi uliopita baada ya kuhudumu kwa mihula miwili.
    Kamati ya Utendaji ya tuzo ya Mo Ibrahim imesema Ellen Johnson Sirleaf ameonesha uongozi wa kipekee katika kukabiliana na changamoto zisizowahi kutokea katika awamu zake mbili za uongozi alipokuwa Rais wa Liberia.

    No comments:

    Post a Comment