• KIBAYACLASSIC

    The voice of Africa

    Wednesday, July 5, 2017

    MAREKANI YAISHUTUMU CHINA KUSHIRIKIANA NA KOREA KASKAZINI


    Rais wa Marekani ameishutumu China kufuatia hatua ya Korea Kaskazini kulifanyia majaribio kombora la masafa marefu, na kuilaumu kwa kuendelea kufanya biashara na Korea Kaskazini.
    Marekani na Korea Kusini zilifanya majaribio ya makombora ya masafa marefu katika bahari ya Japan kujibu hatua hiyo ya Korea Kaskazini.
    China na Urusi wamezitaka pande hizo kuacha kuonyesha ubabe wao wa kijeshi na kusema wanapinga majaribio yoyote ya kubadilisha uongozi nchini Korea Kaskazini.
    Jaribio la kombora ambalo ni la hivi pudne kati ya majaribio kadha, lilienda kinyume na marufuku ya baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa.
    Haki miliki ya mage capti
    Marekani imetaka kufanyika mkutano wa dharura na baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa kujadili suala hilo.
    Trump alifanya mazungumzo na Rais wa China Xi Jinping katika makao yake ya kifahari huko Florida mwezi Aprili.
    Trump alisifu hatua alizopiga na China baada ya mkutano huo.
    Takwimu zinaonyesha kuongezeka kwa biashara kati ya China na Korea Kaskazini.
    Donald Trump and Melania Trump depart for travel to Poland and the upcoming G-20 summit in Germany, from the South Lawn of the White House in Washington, U.S. (July 5, 2017)Haki miliki ya picha
    Image captionRais Trump sasa aneelekea nchini Poland na Ujerumani ambapo atakutana na Bwana Xi kwa mara ya pili.
    Rais Trump sasa aneelekea nchini Poland na Ujerumani ambapo atakutana na Bwana Xi kwa mara ya pili.
    China ambaye ni mshirika mkubwa wa kiuchumi wa Korea Kaskazinia na Urusi, imetaka Korea Kaskazini kuachana na progamu yake ya makombora ya masara marefu.
    Bwana Xi na rais wa Urusi Vladimir Putin waliokutana mjni Moscow siku ya Jumanne walisema pande hizo zinastahili kuanza mazungumzo.

    No comments:

    Post a Comment