• KIBAYACLASSIC

    The voice of Africa

    Tuesday, December 8, 2015

    KIONGOZI WA AL SHABAB AUAWA.

                                       
                                       Kiongozi wa Al Shabaab auawa Somalia

    Kongozi mmoja wa kundi la Al Shabaab ameuawa katika shambulizi la ndege ya Marekani.
    Msemaji wa makao makuu ya ulinzi ya Marekani ,Peter Cook , kifo cha Abdirahman Sandhere ni pigo kubwa kwa usimamizi na uwezo wa mashambulizi ya kundi hilo linalounga mkono wanamgambo wa Al Qaeda.
    Sandhere, anayejulikana pia kama " Ukash'' anadaiwa kuuawa Jumatano iliyopita.
    Al Shabaab inaendesha kampeini ya kuing'oa madarakani serikali inayoungwa mkono na jamii ya kimataifa ilikilindwa na zaidi ya majeshi 22,000 wa umoja wa Afrika.
    Kundi hilo limedhibitiwa katika maeneo mengi iliyokuwa ikikalia.
                               
                                       Kwa mujibu wa duru za ujasusi za Marekani Al Shabaab inakabiliwa na changamoto kwa sababu ya ushawishi mkubwa wa Islamic State na Al Qaeda.
    Hata hivyo kuwepo kwake na tishio la amani imedhihirika kupitia mashambulizi ya kigaidi mjini Mogadishu na vilevile katika taifa jirani la Kenya ambapo wapiganaji wake wametekeleza mashambulizi chungu nzima na kusababisha maafa makubwa.
    Kwa mujibu wa duru za ujasusi za Marekani Al Shabaab inakabiliwa na changamoto kwa sababu ya ushawishi mkubwa wa Islamic State na Al Qaeda.
    Marekani imekuwa ikitekeleza mashambulizi ya ndege zisizokuwa na rubani kuanzia mwaka wa 2011.

    No comments:

    Post a Comment