• KIBAYACLASSIC

    The voice of Africa

    Sunday, October 15, 2017

    MAKUMI WANGAMIA KWA MOTO MAREKANI

    Watu 40 wameuwa na mamia ya wengine hawajulikani waliko baada ya siku sita za moto wa nyika ambao umeharibu maeneo makubwa ya ardhi katika jimbo la California nchini Marekani.
    Gavana wa California anasema kuwa ni moja ya majanga makubwa zaidi jimbo hilo halijawahi kushuhudia.
    Zaidi ya wazima moto 10,000 wanapambana na karibu mioto 16 iliyozalia.


    Prisoners at Oak Glen Conservation Camp leave for work deployment under the authority of Cal Fire on September 28, 2017Haki miliki ya pichaP
    Image captionHata wafungwa wamepelekwa kusaidia kuzima moyo huo

    Upepo unaovuma kwa kasi ya hadi kilomita 70 ulisababisha moto huo kusambaa zaidi na kulazimu watu zaidi kuhama.
    Moja ya maeneo yaliyoathiriwa zaidi ni mji wa Santa Rosa ambapo hadi watu 3000 walihamishwa siku ya Jumamosi.
    "Uharibifu ni mkubwa," Gavana Jerry Brown alisema alipofaya ziara katika mji huo.
    Huo ndio moto mbaya zaidi katika historia ya jimbo hilo. Zaidi ya watu 100,000 wamehamishwa na vijiji vingi vimegeuka majivu
    Moto huo mkubwa umesababisha moshi na majivu hadi anga ya San Francisco, karibu umbali wa maili 50, na hata kwenda miji ya mbali kusini.
    Katika bonde na Naqa takriban viwanda 13 vya mvinyo vimeharibiwa. .Mmiliki mmoja wa kiwanda cha mvinyo huko Santa Rosa anasema moto huo umeharibu mviyo wa mamilioni ya dola.


    Only chimneys remain standing in the fire-ravaged Coffey Park neighbourhood in Santa Rosa, California. October 12, 2017Haki miliki ya pichaP
    Image captionWatu 40 wauawa kwenye moto wa nyika California

    No comments:

    Post a Comment